Saturday, March 8, 2014

Arsenal yaelekea Wembley

Mchezaji wa Arsenal Mikel Arteta

Magoli manne yametosha kuipeleka Arsenal nusu fainali ya FA itakayochezewa katika uwanja wa Wembley. Ikiwa inacheza na Everton mchezo ulionekana kuwa mgumu kwa Arsenal katika kipindi cha kwanza, japo mambo yalibadilika kipindi cha pili baada ya Rosicky na Giroud  kuchukua nafasi za Chamberlain na Sanogo. Arsenal ilikuwa ya kwanza kupata bao kupitia kwa Ozil kabla ya Lukaku kusawazisha katika kipindi cha kwanza. Dakika ya 70 Arsenal ilipata bao la pili kupitia kwa Arteta kwa mkwaju wa Penalt.
Dakika 10 za mwisho Giroud alipachika wavuni magoli 2 na mechi ikaisha ubao ukisomeka 4 - 1.

Kwa habari zaidi tembelea:-

No comments:

Post a Comment